Siha Njema
Katika mkakati wa kupunguza unyanyapaa kwa wazazi wanaowalea watoto wenye Autism shule ya Mali inatoa tiba nasaha na elimu kwa pamoja ikizingatia pia mahitaji ya wazazi wao ambao mara nyingi wanahitaji pia matunzo
Ole ensimmäinen kommentoija
Rekisteröidy nyt ja liity Siha Njema-yhteisöön!
Kokeilun jälkeen 7,99 € / kuukausi. · Peru milloin tahansa.
228 jaksot
Shule ya Mali jijini Nairobi inavyowasaidia watoto wenye Austism pamoja na wazazi
Shinikizo kutaka mataifa kuja na sera endelevu na salama za uchukuzi
Shinikizo zinazidi kutolewa kwa mataifa ya Afrika kukumbatia sera za uchukuzi zilizo salama na endelevu ili kupunguza idadi ya vifo vinavyotokana na barabara na madhara ya ajali za barabara kwa jamii. Katika kongamano la kujadili mpango huo wa usalama ulio endelevu ,wadau wamesikitika vifo vya barabarani bado vinaripotiwa miongoni mwa watembea miguu na waendesha pikipiki. Katika makala ya Siha Njema wiki hii tunajadili kwa nini swala hili ni muhimu kwa ustawi wa jamii.
Majanga yanaweza kusababisha matatizo ya afya ya akili miongoni mwa watoto
Mataifa ya Afrika yameshuhudia mafuriko katika miaka ya hivi karibuni ,hali ambayo imesababisha wananchi wengi kulazimika kuhama makazi yao Nchini Kenya ,ukanda wa magharibi ,katika eneo la Busia,mafuriko hayo yamevuruga kalenda za wanafunzi wa shule ,watoto wengi wakishindwa kuendelea na shule au kukubaliana na msongamano kwenye shule chache ambazo ziko maeneo salama Hali hii imewasababisha changamoto za afya ya akili anavyoeleza mwaandishi wetu Petronila Ogalo.
Mwendelezo wa mlipuko wa Ebola DRC na namna wenyeji wanavyojikinga
Watu 220 wamefariki kwenye mlipuko wa Ebola unaohusishwa na virusi adimu vya Bundibugyo huku wengine zaidi ya 1000 wakiwa wameambukizwa Mlipuko huu hatari umesababisha baadhi ya mataifa kufunga mipaka yake na kuweka masharti magumu ya tahadhari
Kwenye kapu la sekta ya afya kufuatia kongamano la Africa Forward
Baadhi ya makubaliano yalitotangazwa na Ufaransa baada ya siku mbili ya kongamano la Africa Forward ni ufadhili kwa uzalishaji wa dawa na chanjo hapa barani Afrika. Shirika la Unitaid pia lenye ushirikiano na Ufaransa lilitangaza kuratibu mchakato wa kuzalishwa dawa mpya ya kuzuia virusi vya HIV ,Lenacapavir kuzalishwa Afrika Kusini. Na kwenye viungo vingine vilivyosheheni majadiliano ya kuimarisha mifumo ya afya Afrika ni kilimo endelevu .
Kommentit
0Ole ensimmäinen kommentoija
Rekisteröidy nyt ja liity Siha Njema-yhteisöön!