Leider ist dieses Angebot abgelaufen
Starte stattdessen unten deine kostenlose Testversion

Gurudumu la Uchumi
Podcast von RFI Kiswahili
Nimm diesen Podcast mit

Mehr als 1 Million Hörer*innen
Du wirst Podimo lieben und damit bist du nicht allein
Mit 4,7 Sternen im App Store bewertet
Alle Folgen
137 Folgen
Katika bara lenye watu zaidi ya bilioni 1.4, ni watu wanne tu wanaomiliki utajiri zaidi ya nusu ya watu wote. Kulingana na ripoti mpya ya Oxfam, ukosefu huu wa usawa unaostua sio tu takwimu - ni ishara ya wazi ya ukosefu wa haki za kiuchumi uliokita mizizi, mifumo iliyovunjika na kukosekana kwa fursa. Kujadili haya yote nimewaalika Johnson Denge mtaalamu wa uchumi akiwa Nairobi na Apronius Mbilinyi yeye ni mtaalamu wa masuala ya Kodi akiwa Tanzania.

Mwezi mmoja uliopita nilipata bahati ya kuzungumza na Octavian Lasway, mhandisi wa maji na umwagiliaji, lakini pia yeye kijana ambaye anatumia teknolojia kuwasaidia wakulima wa nchi za Afrika Mashariki, kufanya kilimo biashara, kupata masoko na kuongeza thamani ya mazao yao. Huu hapa muendelezo wa mahojiano yetu.

Hivi Leo tunaangazia suala nyeti linalogusa maisha ya mamilioni ya watu katika nchi zinazoendelea hususani za bara la Afrika, kama vile kwenye mzigo wa madeni unaozidi kuwa mzito. Tunajiuliza Nini hasa kiko hatarini? suluhisho gani linapendekezwa? Kujadili hili tunazungumza na Ali Mkimo, mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

Mwezi Juni mwaka 2025, Tume ya Ulaya iliorodhesha Kenya miongoni mwa nchi zenye changamoto ya utakatishaji wa fedha, huku Uganda ikipata afueni kwa kuondolewa kwenye orodha hiyo. Hatua hii ina maana kuwa mashirika ya kifedha – ikiwemo benki – zinalazimika kuzingatia kwa makini uhusiano wa kibiashara na miamala yoyote inayohusiana na nchi zilizo kwenye orodha hiyo, na kuchukua hatua kali za udhibiti wa fedha. Nchi nyingine katika orodha hiyo ni pamoja na Sudan Kusini, Tanzania, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Msumbiji, Nigeria, Afrika Kusini, na zingine. Katika Makala haya, Gurudumu la Uchumi, tunachambua hatua hii na athari zake kwa uchumi, lakini pia nini mamlaka katika nchi hizo zinaweza kufanya hili kujiondoa kwenye orodha hiyo.

Alhamisi ya Juni 12, nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa pamoja kupitia Mawaziri wa Fedha, waliwasilisha Bajeti ya mwaka wa fedha ya mwaka 2025/26. Waziri wa fedha John Mbadi aliwasilisha Bajeti ya Shilingi za nchi hiyo Trilioni 4.2. Bajeti ya Tanzania kwa mwaka huu wa fedha ni Shilingi za nchi hiyo Trilioni 56.49 huku Bajeti ya Uganda ikiwa ni Shilingi za nchi hiyo Trilioni 72.3. Lakini bajeti hii ina maana gani kwa raia wa nchi hizo na je bajeti hizi zinatoa taswira halisi ya mikakati yao nchi hizo kujitegemea na pia kukua? Skiliza makala haya upate ufahamu zaidi tukizungumza pia na David Otieno, mtafiti wa masuala ya bajeti kutoka shirika la Amnesty International.