
Gurudumu la Uchumi
Podcast by RFI Kiswahili
Fahamu masuala kadha wa kadha kuhusu uchumi kama vile, namna ya kupambana na umaskini, mfumuko wa bei, kushamiri kwa matumizi ya dola na athari za kuyumba kwa uchumi wa dunia kwa nchi za Afrika. Mada hizi zinafanyiwa utafiti wa kina na zinazungumzwa kwa lugha rahisi inayoeleweka ili kukufanya uelewe na usichoke kusikiliza .
Aloita 7 vrk maksuton tilaus
Kokeilun jälkeen 7,99 € / kuukausi.Peru milloin tahansa.
Kaikki jaksot
127 jaksot
Msikilizaji wakati dunia ilipoazimisha siku ya kimataifa ya wafanyakazi, viongozi barani Afrika na hasa kwenye ukanda wa Afrika Mashariki walitangaza nyongeza ya mshahara huku wengine wakitoa ahueni ya ushuru wa mapato. Kwenye makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, tunaangazia kodi ya lipa kadiri unavyopata (PAYE) kwa wafanyakazi na waajiri. Kuzungumzia hili msikilizaji kwenye line ya simu nimemualika Ali Mkimo, mtaalamu na mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

Mizozo ya kibiashara kati ya nchi wanachama wa jumuiya za kikanda kama zile zilizoko SADC na EAC, ina athari endelevu kwa uchumi, biashara na jamii kiujumla. Mfano hivi karibuni Tanzania iliingia katika mvutano na nchi za Malawi na Afrika Kusini, zote zikiwa ni wanachama wa SADC, aidha wakati fulani Tanzania, Kenya na Uganda zilishawahi kuvutana. Ali Mkimo mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara anadadavua hili kwa kina kwenye makala ya wiki hii.

Katika juhudi za kuimarisha ubunifu na ushindani wa kilimo biashara barani Afrika, Kenya kwa kushirikiana na Ufaransa zimeanzisha mpango wa mafunzo ya matumizi ya teknolojia kwa wakulima wanawake, yakiangazia Akili Mnemba (AI) kuongeza thamani ya mazao, mpango umefikia zaidi ya vikundi na mashirika 1200 ya wanawake wakulima na kuwawezesha kutumia teknolojia za kisasa kuongeza ubora, usindikaji na masoko.

Msikilizaji kwa majuma kadhaa sasa, kumekuwa na mjadala duniani kote kufuatia uamuzi wa rais wa Marekani, Donald Trump, kutangaza ushuru wa bidhaa zinazoingia kwenye taifa hilo, mataifa ya Afrika yakiwa miongoni mwa waathirika, baadhi wakiwekewa ushuru wa hadi asilimia 50. Hata hivyo juma lililopita, rais Trump alitangaza kusitisha kwa muda wa siku 90 utekelezwaji wa ushuru kwa baadhi ya mataifa isipokuwa Uchina, ambayo imewekewa ushuru wa zaidi ya asilimia 125. Katika sehemu hii ya pili ya makala ya wiki hii, tumezungumza na Ali Mkimo, mtaalamu na mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara.

Kwa majuma kadhaa, mijadala mikali duniani kote kufuatia uamuzi wa rais wa Marekani, Donald Trump, kutangaza ushuru zaidi wa bidhaa zinazoingia kwenye taifa hilo, mataifa ya Afrika yakiwa miongoni mwa waathirika, baadhi wakiwekewa ushuru wa hadi asilimia 50. Katika makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, tunadadavua na wataalamu athari za ushuru wa Trump kwa nchi za Afrika na biashara ya dunia kiujumla. Tutakuwa na Ali Mkimo, mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.
Aloita 7 vrk maksuton tilaus
Kokeilun jälkeen 7,99 € / kuukausi.Peru milloin tahansa.
Podimon podcastit
Mainoksista vapaa
Maksuttomat podcastit